Total Pageviews

Recent news

About Us

Powered by Blogger.

Pages

Wednesday, 20 August 2014

Unknown / / 0
Kushoto ni Padri Kassase akiwa na mkuu  wa chuo cha Mlimani School of Professional Students, Hassani Ngoma katika makabidhiano ya hati ya udhamini wa  wanafunzi .
Viongozi na wawakilishi wa dini ya Kikristo na Kislamu wakiwa katika majadiliano kabla ya mkutano kuanza.
Mkuu wa chuo cha Mlimani Hassani Ngoma akisikiliza maswali kutoka kwa viongozi wa dini (hawapo pichani).
Mkuu wa chuo cha Mlimani School of Profession Students, Hassan Ngoma akikabidhi hati ya udhamini kwa wanafunzi  20 kutoka taasisi za dini ya Kiislam na Kikristo.
Viongozi na wawakilishi wa dini ya Kiislam wakiwa na bahasha zenye fomu ya udhamini walizopewa na chuo cha mlimani School of Profession Students.
Wanafunzi wakiwa wanajisomea eneo la chuo.
Wawakilishi wa dini ya Kikristo na Kiislam zinazozunguka chuo cha Mlimani School of Profession Students, wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa chuo hicho.
Baadhi ya waumini na viongozi wa dini ya Kiislamu wakibadilishana mawazo nje ya jengo la chuo cha Mlimani, Mbezi kwa Msuguri.
Kibao cha chuo cha Mlimani School of Profession Students.
CHUO cha Mlimani School of Profession Students cha Mbezi kwa Msuguri, jijini Dar es Salaam, kimetoa hati za udhamini kwa wanafunzi wasiojiweza wapatao 20, kutoka taasisi za kidini za Kiislam na Kikristo kwa makanisa ya kata tano zinazozunguka chuo hicho.
Kata hizo ni Msigani, Kimara, Saranga, Mbezi na Kwembe zilizopo jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na mwandishi wetu mkuu wa chuo Hassan Ngoma, ameitaka jamii kujitokeza ili kutumia fursa waliyotoa kwa watu waliofeli na wale wenye kipato kidogo kuweza kuwasomesha watoto wao kwa kulipa kiwango kidogo cha fedha kulingana na uwezo wa wazazi ama mlezi wao.
‘’Tumejikita katika kutoa huduma kwa jamii kwa kutoa udhamini wa wanafunzi 20 wasiojiweza, lengo likiwa ni kurudisha fadhila za chuo chetu kuwepo eneo la Mbezi kwa miaka 5,” alisema mkuu wa Chuo hicho.

Unknown


Lorem ipsum dolor sit amet, consectetuer adipiscing elit. Ut odio. Nam sed est. Nam a risus et est iaculis adipiscing. Vestibulum ante ipsum faucibus luctus et ultrices.
Follow me @Bloggertheme9

0 comments:

Recent News