Mtoto wa Mchungaji Mwasumbi, Elizabet Daniel Mwasumbi akilia kwa furaha na kumshukuru Mungu
kwa Muujiza aliyo watendea baada ya tamko la kuachiwa huru kwa baba yake kipenzi
Apostle Jeremiah Mwakanyelenge akisalimiana na wakili Benjamini Mwakagamba ni miongoni
mwa watumishi waliohidhuria kusikiliza kesi ya mtumishi mwenzao
Mtoto wa Mwasumbi na mashuhuda wengine waliokuwa wakifuatilia kwa makini kesi hiyo
Wakili Benjamini Mwakagamba akifafanua jambo mbele ya waandishi wa habri mara tu baada ya kushinda kesi
Mdogo wake na Daniel Mwasumbi mwenye shati la mistari akifuatiwa na katibu mkuu wa kanisa la Uinjilisti Mwakasole mwenye miuani wakisikiliza jambo toka kwa wakili
Hatimaye yametimia
Jaji Atuganile Ngwala aliyetumia muda wa saa 1:15 kusoma hukumu ya kesi iliyokuwwa ikimkabili Mchungaji na Mwimbaji maarufu wa nyimbo za Injiri hapa Nchini Mchungaji Daniel Mwasumbi
Hukumu hii ilitokana na upande wa mtuhumiwa kukata rufaa baada ya hukumu ya awali iliyomtia hatiani mtumishi wa Mungu huyo kwa kuamriwa kutumikia kifungo cha miaka 30 jela. Pamoja na kuchapwa viboko 12 na pia kuawajibika kulipa faini ya Tsh 20,000,000/= pindi amalizapo kutumikia kifungo hicho
Hukumu ya awali iliyopelekea Mchungaji Daniel Mwasumbi (57) kufungwa jele ilitolewa siku ya jumanne ya 2/7/2013 na mahakama ya Wilaya ya Mbeya chini ya Hakimu Gilbert Ndeuruo na serikali kusimamiwa na wakili Achiles Mulisa ambapo mahakama ilimtia hatiani kwa kosa la kukiuka sheria ya nchi kifungu cha 130 (2) e na 131 (1) sura ya 16 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2002
Wakili wa kujitegemea aliyekuwa akimtetea Mchungaji Daniel Mwasumbi ambaye alikuwa anakabiriwa na mashitaka makubwa mawili Kubaka na Kumpa mimba mwanafunzi
ilisadikiwa kuwa Mchungaji alitenda kosa hilo kati ya mwaka 2008 hadi 2011 ambapo katika kipindi hicho alimpa mimba binti huyo Neema Ben (19) mwanafunzi wa shule ya Sekondari Itende na kubahatika kupata watoto wawili kati ya 2008 na 2011. Kilichopelekea Mtumishi wa Mungu Mwasumbi anayetamba na nyimbo kama Dhambi ni mbaya na nyingine nyingi kufungwa jela
Lakini baada ya hukumu hiyo upande wa mtuhumiwa haukuridhika na mwendo wa kesi pamoja na hukumu hiyo. Waliamua kukata rufaa 26/7/2013 na shauri lake kusomwa mahakamani 3/11/2013 chini ya wakili wa kujitegemea Benjamini Mwakagamba kutoka Dar es Salaam, wakati upandea wa Serikali ikiwa chini ya wakili Prosister Paul
Upande wa utetezi ukiwa na hoja kwamba kulikuwa na ukiukwaji wa kisheria katika hukumu hiyo
Jaji Atuganile Ngwala akisoma hukumu hiyo alisema utoaji hukumu hiyo haukuzingatia vipengele muhimu vya kisheria vilivyotumika kumtia hatiani Mchungaji Mwasumbi
Katika rufaa hiyo kuna mambo kadha wa kadha ambayo yalonekana kukiukwa katika kutoa hukumu hiyo kama alivyoweza kubainisha wakili wa utetezi hivyo jaji kasema nakubaliana na wakili wa upande utetezi Mwakagamba kuwa kulikuwa na ukiukwaji wa kisheria katika hukumu hiyo
Kama ilivyoelezwa na wakili msomi na mwenye weredi katika kazi hiyo ya kisheria Bwana Mwakagamba kuwa muda lilipotokea tukio na liliporpotiwa kwenye vyombo vya usalama unaonekana kuchelewa na kukinzana na zaidi sana ushahidi uliotolewa mahakamani na mhanga wa tukio hilo ulionekana kujichanganya na kuonesha wazi kuwa mtuhumiwa hakutenda kosa hilo
Lakini jaji Ngwala alitoa kali yenye kuaktisha tamaa kwa upande wa mtuhumiwa pale aliposema kuwa mtu kama huyu ni mende na mtu hatari katika jamii, hivyo anastahili kudhalilishwa na kuadhibiwa. Kitu kilichifanya wote wliohudhuria kusikiliza kesi hiyo kwa upande wa Mchungaji kukata tamaa na kuinamisha nyuso zao chini
Jaji aliendelea kusoma hukumu kuwa kutokana na mwendo wa kesi husika kujikanganya kwa ushahidi na zaidi sana shahidi namba 1 mhanga mwenyewe
jaji karejea kauli yake kusema mende hafai ni hatari katika jamii na hakustahiri katika jamii kama ingethibitika na ushahidi kuthibitisha, lakini kwa kuwa ushahidi umeshindwa kuthibitisha hilo hivyo basi mtuhumiwa ana haki kisheria ya kuachiwa huru.
Jaji Atuganile Ngwala akahitimisha kwa kusema upande wa Jamhuri chini ya wakili makini katika kazi yake Prosisteer Paul kuwa una haki ya kukata rufaa na kesi kuanza upya endapo haujaridhika na hukumu hiyo
Wakili
aliyekuwa akimtetea Mchungaji Mwasumbi alisema kuwa katika rufaa ya mteja wake
aliwasilisha sababu saba za kupinga hukumu hiyo ambapo alidai kuwa hakimu
wakati wa kutoa hukumu hiyo alikosea kisheria na haki muda wa kuripotiwa kwa
shauri hilo kwa vyombo vya usalama na lilipotokea ulikinzana na kwamba
aliegemea kwa ushahidi wa Mhanga tu.
Sababu
zingine alidai kuwa hakimu aliegemea katika ushahidi au vidhibiti ambavyo
awali alivikata mwenyewe, pia alidai kuwa hakimu hakuangalia uhalisia kosa
lenyewe na badala yake alionekana kutoa maoni yake binafsi.
Lakini
sababu nyingine wakili Mwakagamba alisema kuwa hakimu huyo, aliegemea ushahidi
ambao ulijichanganya, wendesha mashtaka walishindwa kuwapeleka mahakamani
hapo mashahidi wa msingi katika kesi hiyo, hakimu aliegemea upande wa
vyeti vya watoto wawil waliodaiwa ni wa Mchungaji Mwasumbi ambapo vyeti
vilidurufiwa (photocopy) na si vyeti halisi na mwisho hakimu huyo alitoa
hukumu ambayo haikufuata mtiririko uliosahihi wa mashahidi husika.
Akizungumza
na waandishi wa habari, mtoto wa Mchungaji Mwasumbi, Elizabeth Mwasumbi
alisema anamshukuru Mola kwa kumwezesha Jaji Ngwala kwa kutenda haki katika
rufaa ya baba yake.
Alisema;
’Mimi na wenzangu tulikuwa na wakati mgumu sana pindi baba yetu akiwa ndani,
kwani mimi niliathirika sana kiafya na kiuchumi nilishindwa kufanya shughuli
yoyote kutokana na mawazo lakini namshukumuru Mungu kwa kutenda haki’.
Na Eliezer Masoud
Apostle blog





%2B(1).png)
Amen
ReplyDelete