Total Pageviews

Recent news

About Us

Powered by Blogger.

Pages

Thursday, 8 May 2014

Unknown / / 0

KWA TAARIFA YAKO : HII NDIO SIRI YA SOLO MAARUFU WA KINONDONI REVIVAL CHOIR

Haya msomaji wetu wa Gospel Kitaa karibu katika kipengele chetu maalumu ''KWA TAARIFA YAKO'' ambacho kinakujia kila siku za alhamisi ndani ya GK kikiwa na lengo la kukupatia habari ambayo iliwahi kutukia lakini yawezekana huijui pia yawezekana ilitukia ukawa unaijua lakini GK ikawa imesahau mahali au kuna sehemu haina usahihi utapata fursa ya kusahihisha kwa kuweka comment yako chini kabisa kwenye habari husika. Karibu



"Kwaniniii wataka kujiua wewe? kwaninii huna hamu ya kuishi? elimu unayo lakini huna amani, dini yako nzuriii lakini huna amani" haya ni baadhi ya maneno ya moja ya wimbo maarufu wa kwaya ya Kinondoni Revival kutoka Assemblies of God Kinondoni kwa Askofu Rogathe Swai. KWA TAARIFA YAKO hii leo ni kukujuza kuhusu mwimbaji solo wa muda mrefu wa kwaya hiyo ambaye uimbaji wake umekuwa kama kitambulisho cha kwaya hiyo popote aendapo. Huyu si mwingine bali ni mwanadada Rebecca Nzelwa Lukule ambaye kwasasa ni mke wa mtu.

KWA TAARIFA YAKO Rebecca ameimba nyimbo nyingi sana na kwaya ya Revival kati ya nyimbo hizo ni pamoja, Twaililia Tanzania ambao ndio uliomtambulisha vyema kwenye huduma ya uimbaji na ndio wimbo wake wa kwanza kuutengenezea solo (walipewa ruhusa na mwalimu wao kila mwimbaji atengeneze solo ya kujazia wimbo huo ) ambayo ilipitishwa na mwalimu wa kwaya kwamba aimbe kama alivyotengeneza. KWA TAARIFA YAKO Rebecca ambaye ni miongoni mwa waanzilishi wa kwaya ya Revival toka amejiunga nayo mwaka 1993 wakati huo kwaya nyingine ya kanisani hapo iitwayo Victory Singers walikuwa wakivuma haswa katika muziki wa injili.



KWA TAARIFA YAKO Rebecca aliendelea kuvumisha injili kupitia nyimbo zilizopata umaarufu kama 'Vumilia Samweli atazaliwa' na Mtu wa nne nyimbo ambazo Mungu ametenda makuu kwa watu wake na shuhuda nyingi kuwafikia wanakwaya hao "wako watu ambao hawakuwa na watoto lakini Mungu amewapa watoto, Wako ambao wamekuwa wakipitia mambo magumu lakini Mungu amewatetea na mambo mengi zaidi ya hayo" Rebecca ameiambia GK. KWA TAARIFA YAKO kujishusha kwake na uimbaji wake hodari Rebecca alichaguliwa na waimbaji wenzake kuwa mwalimu msaidizi wa kwaya akishirikiana na kupewa msaada na mwalimu mkuu wa kwaya kutengeneza nyimbo.
KWA TAARIFA YAKO kama hujui Rebecca ameichukulia umakini huduma ya uimbaji kwakuhakikisha anasimama imara katika maombi kuiombea huduma ya kwaya yake na yeye binafsi KWA TAARIFA YAKO kama hujui Rebecca kwasasa amehama kimakazi yupo jijini Arusha na mumewe ambaye Rebecca anasema anampa sapoti kubwa katika huduma yake ya uimbaji hata sasa wanaabudu katika kanisa la Assemblies Bethel Christian Centre kwa askofu Oral Sossy "Bado naendelea kumtumikia Mungu, na mwaka huu nimeamua kumtumikia Mungu na kwaya ya inayoitwa Bethany ambapo nimeweza kuimba nao wimbo unaoitwa "Mungu wetu hachoki" na tayari kwaya imetoa DVD yao inayoitwa "Wewe ni Mungu wa kweli"
kila asimamapo kuhudumu ili Mungu akapate kusema na watu wake, na matokeo yake yameonekana kupitia shuhuda hizo ambazo zimekuwa zikiwafikia kutoka kwa watu ambao wamepata nafasi ya kuhudumiwa na kwaya hiyo.
KWA TAARIFA YAKO Mimi binafsi pia bado naendelea kufanya huduma mbalimbali nimeendelea kupata mialiko ya kuimba ndani na nje ya nchi na nina watu ambao tumeamua kujiunga pamoja ili kufanya huduma hii. Tunatembelea watoto yatima kuwafariji na kuwahudumia, tunatembelea watoto wa mitaani na kubadilisha mwelekeo wa maisha yao na tunaendelea kujifunza kuimba na kutembea na Mungu na kumcha Mungu" Wiki ya pasaka nilialikwa Nairobi Easleigh kuhudumu kwenye kongamano la wachungaji na watumishi mbalimbali wa Mungu. Hii inanipa kusonga mbele kwenye utumishi na hata maisha ya kiroho kuwa bora zaidi" Rebecca ameiambia GK.
KWA TAARIFA YAKO kama hujui siri ya mafanikio ya Rebecca kupendwa na wengi katika huduma yake ya uimbaji, ni kwamba kuna mengi ayafanyayo ukiacha mazoezi ya uimbaji lakini pia ametabanaisha siri yake kupitia GK kwamba "Naendelea kujifunza kutoka kwa Mungu, nataka uimbaji KWA TAARIFA YAKO hiyo ndiyo siri inayomfanya Rebecca kuwabariki wengi kila asimamapo madhabahuni kumtumikia Kristo.
unaobadilisha maisha ya watu, nataka uimbaji wenye mguso, hii inawezekana hivyo nimeamua kuishi na kutembea na Mungu ili nimsikie kiumakini anataka nini kwenye maisha yangu na kwenye utumishi huu. Ninachokiimba nimaanishe, maisha ninayoishi nje ya madhabahu yawe ni kama ninaposimama madhabahuni".
Hiyo ni KWA TAARIFA YAKO kwa leo, vinginevyo tukutane wiki ijayo….

Unknown


Lorem ipsum dolor sit amet, consectetuer adipiscing elit. Ut odio. Nam sed est. Nam a risus et est iaculis adipiscing. Vestibulum ante ipsum faucibus luctus et ultrices.
Follow me @Bloggertheme9

0 comments:

Recent News