Huku wataalamu wakionya kuwa kiwango cha maambukizi huenda kikawa watu 10,000 kwa wiki ifikapo Desemba, watafiti kote duniani wanang'angana kutafuta suluhisho la kuudhibiti ugonjwa huo ambao kwa wakati huu hauna tiba au chanjo iliyoidhinishwa rasmi kupambana nao.
Wakati huo huo, chanjo ya majiribio ya rVSV dhidi ya Ebola imewasili katika chuo kikuu cha Geneva kutoka Canada.WHO itaratibu majaribio ya chanjo hiyo sambamba na chanjo nyingine zinazofanyiwa majaribio Ujerumani, Gabon na Kenya.
Naibu mkurugenzi mkuu wa WHO Marie Paule Kieny amesema lengo ni kusafirisha chanjo kuelekea Afrika ifikapo mapema mwaka ujao ili kuanzishwa kwa kampeini kubwa ya kutolewa kwa chanjo hiyo ambayo bado haijaorodheshwa katika kadi za chanjo.
Hayo yanakuja huku Marekani ikiimarisha madurufu uchunguzi wa kimatibabu kwa wasafiri wanaotokea nchi za magharibi mwa Afrika zilizoathirika na Ebola na kutangaza wasafiri hao watalazimika kufanyiwa uchunguzi wa kina kwa siku ishirini na moja.
Rais wa Marekani Barrack Obama amesema kukiwa na mifumo muafaka Ebola inaweza kudhibitiwa kama ilivyokuwa Senegal na Nigeria
Na Liberia imeanza kutumia mfumo wa kuwianisha taarifa za jamaa ili kuzuia wasafiri ambao wana jamaa zao waliogua Ebola hata kama hawana dalili za maambukizi kutosafiri nje ya nchi hiyo ili kupunguza kuusambaza ugonjwa huo katika nchi za kigeni.
Rwanda nayo imefutilia mbali vikwazo ilivyokuwa imeweka dhidi ya wasafiri kutoka Marekani na Uhispania kama njia mojawapo ya kuzuia Ebola kuingia nchini humo.
Waziri wa afya wa Rwanda Agnes Binagwaho wiki hii aliagiza wasafiri wote kutoka Marekani na Uhispania kuifahamisha wizara yake kila siku kwa wiki tatu ambazo watakuwa nchini humo hali yao ya kiafya baada ya visa vya Ebola pia kuripotiwa katika nchi hizo mbili.
Taarifa kutoka kwa Rais Paul Kagame hata hivyo imesema agizo hilo limefutiliwa mbali kwani haihitajiki na kuongeza waziri huyo saa nyingine huchukua hatua za haraka na kufikiri baadaye badala ya kuwa vinginevyo.
Wasafiri kutoka Guinea,Liberia na Sierra Leone wamezuiwa kuingia Rwanda na raia wake ambao wamesafiri katika nchi hizo tatu wanawekwa karantini kwa siku ishirini wanapowasili.
%2B(1).png)
0 comments: