Total Pageviews

Recent news

About Us

Powered by Blogger.

Pages

Tuesday, 22 July 2014

WADAU WA ELIMU WAOMBWA KUCHANGIA MAENDELEO

Unknown / / 0



Kutoka kushoto ni Mkuu wa Shule ya Sekondari Sangu, Mwalimu, Andongwisye Bukuku, Katibu wa Jumuiya ya wazazi, wilaya  ya Mbeya Mjini, Juma Mng'ombe na Mkuu wa shule msaidizi Sophyllin Gwandage.
 Katibu wa Jumuiya ya wazazi, wilaya ya Mbeya mjini, Juma Mng'ombe.
 Mkuu wa shule msaidizi, Sangu sekondari, Sophyllin Gwandage akiwa ofisini kwake.
 Mkuu wa Shule ya Sekondari Sangu, Mwalimu, Andongwisye Bukuku.

 Wanafunzi wa kidato cha tatu mchepuo wa Sayansi 1&2.



WADAU wa Elimu Nchini wameombwa kujitokeza kuchangia maendeleo ya kielimu katika kuhakikisha wanafunzi wanapata mazingira mazuri ya kujifunzia, ikiwa ni pamoja na walimu kufundishia.
Katika kuhakikisha wanafunzi wanapata mazingira bora ya kujifunzia, shule ya sekondari SANGU inayomilikiwa na Jumuiya ya wazazi ya Chama Cha Mapinduzi(CCM), iliyopo Jijini Mbeya, imeandaa harambee kwa ajili ya ujenzi wa maabara kubwa ya kisasa na ununuzi wa usafiri wa basi la wanafunzi. 

Akiungumza na waandishi wa habari jana, Mkuu wa shule hiyo, Mwalimu Andongwisye Bukuku, alisema Maabara hiyo inatarajia kugharimu kiasi cha Tsh.111,000,000/=, wakati basi la shule litagharimu shillingi milioni 50.

Alisema ujenzi wa maabara hiyo utasaidia kwa kiasi kikubwa uwepo wa wanafunzi watakaosoma masomo ya sayansi,  na kuongeza kuwa wanafunzi waliopo kidato cha tano na sita ni wale wenye michepuo ya sanaa (Art) pekee, hivyo upatikanaji wa maabara hiyo utatoa fursa kwa shule hiyo kuanzisha michepuo ya sayansi na wanafunzi kunufaika.

“Harambee hii tunatarajia kuifanya Agost 14, mwaka huu, katika ukumbi wa Mkapa hapa Mbeya, ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Naibu Waziri wa Fedha, NDG.ADAM KIGOMA MALIMA, ambapo matarajio yetu ni kupata shilingi milioni 161.

Kwa upande wake katibu wa Jumuiya ya Wazazi (CCM),wilaya ya Mbeya mjini, Juma Mng’ombe, amewaomba wadau wote kujitokeza kwa wingi siku hiyo, kuunga mkono jitihada hizo hususani wanafunzi wote waliosoma shuleni hapo miaka ya nyuma.

Amewataja baadhi ya watu waliosoma shuleni hapo kuwa ni Rais wa Jamhuri ya watu wa Demokrasia ya Kongo, Joseph Kabila, Mbunge wa Sindgida mjini, Azam Dewji na mbunge wa jimbo la Songea Mjini Emmanuel Nchimbi.

Aidha,Mng’ombe amewaalika wadau wote wenye mapenzi na elimu kote nchini kuchangia kupitia akaunti namba iliyoanzishwa mahususi kwa ajili ya harambee hiyo…..

CRDB bank Tawi la Mbeya. 01J1065276501

Unknown


Lorem ipsum dolor sit amet, consectetuer adipiscing elit. Ut odio. Nam sed est. Nam a risus et est iaculis adipiscing. Vestibulum ante ipsum faucibus luctus et ultrices.
Follow me @Bloggertheme9

0 comments:

Recent News