MUNGU ALITENDA ANATENDA NA ATATENDA MVUA ZA BARAKA KWA WATU
Dalili za mvua ya baraka kunyesha ni kubwa sana.
Ni katiak semina kubwa ya Neno la Mungu inayaoendelea Kyimbila Tukuyu ambapo mkufunzi wa semina hiyo Apostle Jeremiah Mwakanyelenge anafundisha na kuombea watu wenye shida mbalimbali
Apostle Jeremiah Mwakanyelenge akifundisha mamia ya watu wanao hudhuria semiana inayoendelea Kyimbila Moravian
Fuatilia matukio haya katika picha
kwaya ya wenyeji wakimsifu Mungu
mama ambaye alikuwa hawezi kutembea bila kutukia fimbo lakini baada ya kufanyiwa maobezi mama akiwa na furaha iliyoje huku akionesha fimbo yake juu sasa mateso basi tena Mungu huyu
Semina hii imebeba kichwa cha somo Tengeneza madhabahu ili mvua ya baraka inyeshe. kadri semina inavyo zidi kuendelea na leo ikiwa ni siku 4 tangu semina kuanza hakika tunaona wingu zito la mvua za baraka limetanda kuashiria kunyesha kwa mvua za baraka hata kabla siku 8 hajaisha
hakika tuna muona Mungu akitenda mambo makubwa mmno miujiza inatendeka hakika Mungu ni mwema sana kwetu
Katika kufafanua somo hilo Apostle Jeremieah ameainisha maana saba za namna ya kuitengeneza madhabahu ambapo mamia ya watu wanaohudhuria semina hii wamejikuta wakifunguliwa macho yao na kuona kumbe wamejitengenezea madhabahu zingine nje ya madhabahu yenye uhusiano na Mungu na ndiyo maana watu hujikuta wakishindwa kubarikiwa na kujikuta wakikalia laana
Waweza jiuliza maswali kuwa mvua za baraka ni zipi hizo tena. Ni mafanikio ya Rohoni na mwilini ambayo ni haki yetu kupata toka kwa Bwana maana tuwarithi wa ufalme wake. ikwa ni pamoja na amani, furaha, afya , mali
tutaendelea kukujuza kinachoendelea ama zaidi sana tafuta DVD za semina hii na nyingine nyingi
uliza hapa 0754637974
No comments:
Post a Comment