Total Pageviews

Recent news

About Us

Powered by Blogger.

Pages

Monday, 9 June 2014

JAMANI JAMANI KIMENUKA TENA MBEYA WANANCHI WA MBEYA WAPATA SHIDA

Unknown / / 0
Hiki ni kituo cha daladala cha Kabwe ambacho ni kituo kikubwa cha daladala kwa jiji la Mbeya kikiwa hakina msogamano wa magari baada ya daladala za Uyole - Sokomatola/ Stend kuuu/ Majengo kugoma
Kituo kikiwa cheupe hakina daladala yoyote ya kuelekea Uyole huku abiria hawamini macho yao
Abiria wakiwa kstika nyuso za huzuni kwa kutokuwa na usafiri wa uhakika kuwapeleka katika majukumu ya kila siku huku Bajaji zikiokoa jahazi ama ndo vile tena kuvunjika kwa pakacha nafuu ya mchukuzi
Hatimaye kufa kufana kila aina ya gari lenye uwezo na nafasi ya kubeba ilibeba abiria ikiwa inashusha na kupakia abiria katika kituo cha kabwe
Bajaji zikiwa kazini huku waendesha bajaji wakiomba hali hii iendelee hata kwa wiki baada ya kunufaika na mgomo huo

Mwenye Noah, Canter, Fuso, Pikipiki kaingiza barabara kuokoa JAHAZI baada wenye Hiace kuibip serikali

Bora kufika haijarishi uko katika usafiri wa aina gani
 Kituo cha Mwanjelwa chenye pilikapilika nyingi leo kikiwa cheupe kabisa
Watu wakikimbilia Canter ndo usafiri wa siku ya leo
Wamama wakihangaika wenye nyuso za huzuni katika vituo
Leo 9/6/2014 imekuwa ni asubuhi yenye mchanganyiko wa huzuni na furaha manung'uniko na pongezi kati ya makundi kadha wa kadha baada ya daladala kugoma kutoa huduma ya usafiri kutoka Uyole kuelekea Sokomatola, Stend kuu na Majengo kugoma kutoa huduma kwa siku ya leo

Madai yao makubwa ni kupinga njia zilizoongezwa ya kuzunguka Moondust Uhai Batist na kutokea Soweto stendi kwa gari zinazo tokea mjini kuelekea Uyole wakati zile za kutokea Uyole zinakunja kutokea Soweto kupitia njia ya Chuo kikuu cha Teku Block T na hatimaye kutokea Kabwe.

Wanadai kuwa hizo njioa zifutwe ili wapite njia kuu kusiwepo na mchepuko ama nauli ipandishwe hadi 500/= waameona hii ni njia ya kuishinikiza SUMATRA kubadilisha mfumo uliopo wa kutoa huduma hizo za usafiri

Jambo la msingi tunasaha kuwa kukua kwa jiji lazima kutalazika kuongezeka kwa njia ili kuendana na ongezeko la idadi ya magari kupanuka kwa mji si vema kuishi kwa mazoea tukubali kubadilika

Lakini ndo hivo tena wengine wananufaika na mgomo huo kwa kujiongezea kipato kama vile Bajaji Picup kubeba abiria kama unavoona kwenya picha hapo juu

Lakini hebu tuone katika sakata hili serkali itasema nini na je hawa watoa huduma watalegeza msimamo wao ama wataendelea na msimamo huo huo tutajua mwisho wake
Tutaendelea kukupa kinacho jili
 By M Eliezer

Unknown


Lorem ipsum dolor sit amet, consectetuer adipiscing elit. Ut odio. Nam sed est. Nam a risus et est iaculis adipiscing. Vestibulum ante ipsum faucibus luctus et ultrices.
Follow me @Bloggertheme9

0 comments:

Recent News